Sunday, March 25, 2018

MADHARA YA UMWAGAJI DAMU KATIKA NCHI (KIBIBLIA)

“…kwa kuwa damu huitia nchi unajisi; wala hapana sadaka itoshayo kwa ajili ya nchi, kwa ajili ya damu iliyomwagwa ndani yake…” (Hesabu 35:33)

Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe,
Utangulizi

Tunamtukuza Mungu Baba yetu kwa neema aliyotupa kupitia Mwana wake pekee Yesu Kristo kutupa nguvu za Roho wake Mtakatifu ili tupate kuyatafakari maandiko pamoja. Leo tunaangalia suala moja muhimu sana katika uhai na ustawi wa taifa (nchi), nalo ni: Madhara ya umwagaji damu katika nchi. Msitari tuliouweka hapo juu unatupa mahali pa kuanzia katika kulitafakari suala hili muhimu. Ili tuende pamoja vizuri katika somo hili, ngoja tuangalie mistari kadhaa katika Biblia.

Friday, October 13, 2017

ADHABU YA AMANI

Mwandishi: Anderson Leng'oko

Isaya 53:5
Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Kitabu cha Isaya kinaitwa kitabu cha agano jipya katika agano la kale. Kitabu hiki kinaongelea sana habari za Yesu katika agano la kale kuliko vitabu vingine vyote vya agano la kale. Kitabu cha Isaya kipo katika kundi la vitabu vya kinabii, kwa hivyo maneno mengi yanayoongelewa humo yanatabiri mambo yatakayotokea hapo baadaye. Hivyo hilo suala linaloongelewa hapo juu lilikuwa ni suala la kinabii ambalo lilikuwa halijatokea wakati kitabu kinaandikwa; bali nabii aliona katika Roho mateso ya Bwana Yesu hivyo akawa anayasema kama tulivyoona hapo juu kwenye huo mstari.

Kwa hivyo kabla hatujaendelea natamani tuelewe hapo kuwa ingawa ni katika agano la kale, huo mstari hapo juu unamuhusu Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye hai. Yesu alikuwa na mambo mengi aliyoyafanya na yaliyotokea katika maisha yake, na hapo huo mstari unaongelea mateso yake aliyoteswa kwa ajili ya dhambi zetu ili sisi tupate kuokolewa.

 Yesu alijeruhiwa na kuteswa ili sisi tupate amani. Kile alichopitia Biblia inakiita ‘adhabu ya amani yetu.’
Adhabu ni nini basi? Adhabu ni kitu anachopewa mtu, au anachofanyiwa mtu pale anapokuwa amekosea.
Je, Yesu alikuwa amefanya kosa gani? Yesu alikuwa hana kosa; alikuwa amethibitishwa kuwa hakuwa ametenda dhambi, wala kosa lolote lililokuwa linasababisha afe/ahukumiwe kufa.

Yohana 19:4
Kisha Pilato akatokea tena nje, akawaambia, Mtu huyu namleta nje kwenu, mpate kufahamu ya kuwa mimi sioni hatia yo yote kwake.

Friday, September 22, 2017

UNAFANYA ZIADA GANI? (SEHEMU YA NNE)

  

Mwandishi: Anderson Leng'oko

ZIADA YA MSAMARIA MWEMA

Utangulizi
Kwa neema ya Mungu bado tuna vitu tunavijadili kuhusu kufanya ziada, na leo tunakijadili kisa maarufu cha Msamaria mwema. Karibu ujifunze nasi, na kama hujasoma sehemu zilizotangulia na ungependa kupata mtiririko mzuri bonyeza hapa.

Luka 10:30-35
Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang'anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.

Hii ni hadithi ambayo husomwa na inajulikana sana, inaitwa hadithi ya Msamaria mwema. Katika historia, watu wa Samaria(wasamaria) na watu wa Yuda(wayahudi), walikuwa hawapendani kabisa na chuki yao ilifikia hadi hatua ya kutokupeana hata maji ya kunywa.

Yohana 4:7-9
Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.
Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

Tuesday, August 8, 2017

UNAFANYA ZIADA GANI? (SEHEMU YA TATU)




 Mwandishi: Anderson Leng'oko
 
Utangulizi
Yesu ndiye chanzo cha mafundisho ya kanisa; kila neno tujifunzalo lazima liwe na msingi wake katika mafundisho ya Yesu, kwani yeye ndiye hasa aliyetumwa kuja kuishi ili kwa maisha yake tuone ni kwa namna gani tunaweza kumuishia Mungu. Tuangalie kile Yesu alichokisema kuhusu kufanya ziada ili tuendelee kuona ni uelekeo gani hasa kama kanisa tunatakiwa kuwa nao. 
Kama hukusoma sehemu zilizotangulia katika somo hili bonyeza hapa ili upate mtiririko mzuri.


Tutafakari mistari ya Yesu, kwa undani tukahusianishe na somo hili

Mathayo 5:48
Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

Yesu anatamani tuwe wakamilifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyo mkamilifu. Hii inamaanisha kwamba yale yote ambayo Baba yetu wa mbinguni anayafanya kwa wema wake tunatakiwa kumuiga na kuyafanya vilevile; na hayo yanajumuisha aliyoyataja Yesu ya kuwanyeshea mvua waovu na wema na kuwaangazia jua. Na sisi pia tunatakiwa kuwasaidia na kuwahudumia wakosefu sawasawa na waaminifu na kuwapenda wote pasipo kubagua.